Featured Posts

KARIBU KATIKA WEBSITE YETU, AMBAYO INAHUSU NENO LA MUNGU. UNA KARIBISHWA KUTOA MAONI YAKO YOYOTE YATAKAYO WEZA KUTUKUTANISHA WANAWOTE WA MUNGU KWAPAMOJA. NAWASIHI KILA MMOJA WETU AJIHESHIMU KWA KUTUMIA LUGHA ZINAZOELEWEKA.

Friday, January 3, 2020

NEW LIFE IN CHRIST - ( MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO )

Posted by Savior Ministry at 2:06 AM 0 Comments


2 #Wakorintho 5:17-18
[17]Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.[18]Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho;
Nilipokuwa mchanga kwenye wokovu, niliambiwa haya ni matokeo ya Rohoni
( kuwa kiumbe kipya ) na hayako mwilini.
Inaweza kuwa ni kweli yenye Degree Fulani
( lakini kuna kweli kubwa zaidi ya Hii )
Kama huyu mtu amekuwa kiumbe kipya
Upya wake hautaonekana rohoni kwa macho ya nyama, kwasababu Watu hawawezi kuiona roho ila wanauona mwili , sasa yatakuwaje maisha mapya, atakuwaje kiumbe kipya kama mabadiliko hatutayaona mwilini ? Na Biblia inasema #Mathayo 5:16
[16]Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.
Upya huu una mabadiliko ya Jumla
Siku ileile mtu anapookoka ( Roho inapopokea upya, inapeleka taarifa ya mabadiliko sekunde ileile mwilini ). Ndio maana mtu akiokoka siku hiyo , ukimwambia ukazini atakataa, kwasababu hata mwili wake unaitikia mabadiliko.
Luka 19:8-9
[8]Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.
[9]Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.
Haya ni mabadiliko ya Zakayo baada ya kumpokea Yesu, ni siku hiyo hiyo , siku hiyo hiyo akawa mtoaji, siku hiyo hiyo kajua faida za kuwapa maskini, siku hiyo hiyo akaona sio vyema kukaa na vitu vya utapeli na unyang'anyi
Yesu akadhibitisha kuwa #Kweli wokovu
Umeingia #Ndani yake na nyumbani kwake.
( Haya yalikuwa ni mabadiliko ya Jumla)
Kwa mfano huu wa Zakayo utajua kuwa
Siku Mtu ameokoka kunakuwa na mabadiliko
Ya moja kwa moja kwenye Roho, Nafsi na Mwili.
KUNA KITU HUWA NAKIKATAA
mfano mtu ameanguka dhambini halafu
Watu wanasema ni mchanga kwenye wokovu,
Huu ufahamu sio mzuri sana endapo ukipewa kipaumbele.
Kwa mtu aliyeiamini kweli kwa kupokea injili ya kweli yenye uvuvio wa nguvu za Roho wa Mungu na akapokea mabadiliko kutokea kwenye maamuzi yake yaliyozaliwa na imani yake kwa Bwana Yesu ( Hawezi kufanya dhambi tena). Huyu ni kiumbe kipya.
ANGALIA HUU MSTARI KWA UMAKINI
2 #Wakorintho 5:17-18
[17]Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita #tazama! Yamekuwa mapya.
Ya kale yamepita #Tazama ! Yamekuwa Mapya
( angalia nyakati - Biblia inasema yamekuwa)
Uzito wa mstari huu ni haya maneno
#TAZAMA
#YAMEKUWA
Huyu mtu amekuwa kiumbe kipya
Mambo ya kale yamepita
Mambo gani ya kale
" Uongo , husuda, kutokusamehe, ugomvi, tamaa, wivu, ulevi , usengenyaji, uzinzi n.k "
Haya mambo biblia inasema yamepita ( sio yatapita baada ya kukaa kwenye wokovu miaka 3) , sio yatapita akianza kuhudhuria kanisani, No Biblia imesema yamepita. Haya mambo sio sehemu ya maisha mapya hata asilimia 0.000001
Biblia inasema #TAZAMA
( Hili Neno ndio limebeba maana ya Mstari kwa ujumla), Maana usipotazama " hutaona matokeo yeyote japo tayari yamekuwa mapya tayari.
TAZAMA ! YAMEKUWA MAPYA
Kuna maana kwanini Mtume Paulo alisema #TAZAMA, kiingereza imetumia Neno Behold " likiwa na maana kukiangalia kitu kwa muda na kwa umakini mpaka upate fundisho au ufahamu juu hicho kitu.
Hicho ndicho kinachosemwa kwenye kitabu cha mithali ; Mithali 24:32
[32]Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana;
Naliona, nikapata mafundisho.
Ukitazama Na Kufikiria ukajua Yesu alisema IMEKWISHA
Yohana 19:30
[30]Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema,#Imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake.
IMEKWISHA " maana yake nimekwisha kushughulikia chanzo cha anguko la mwanadamu, kwahiyo sasa mnaweza kuishi maisha huru"
Kama Bwana Yesu alikwisha kuishughulikia dhambi basi inawezekana kuishi mbali na husuda , chuki, visasi, uzinzi, tamaa
Ndio maana Biblia inataka UTAZAME
ufikirie kwa undani kile ambacho tayari Bwana
Yesu alikwisha kufanya kwa ajili yako UTAJUA KUWA yote yamekuwa mpya.
KUBWA KULIKO
Baada ya kutazama na kuona kuwa yamekuwa mapya Biblia inasema [18]Lakini vyote pia #vyatokana na Mungu,
VYOTE VYATOKANA NA MUNGU
baada yakuokoka na kuwa kiumbe kipya #SASA mambo yote yanatokana na Mungu
Afya yako haitokei kwenye dawa, Afya yako inatokana na Mungu , Ndoa yako inatokana na Mungu, Uchumi wako unatokana na Mungu , masomo yako yanatokana na Mungu, Huduma yako inatokana na Mungu ( HAKUNA TENA UGUMU WA MAISHA - KWASABABU VYOTE VYATOKANA NA MUNGU)
Unaacha kujitumainia mwenyewe unaanza kumtumaini Mungu aliyeweka Upya kwenye kila eneo.
Kuwa na Afya inakuwa jambo rahisi, kufanikiwa inakuwa jambo rahisi , Kuoa au kuolewa inakuwa jambo rahisi, Kuishi maisha maisha matakatifu inakuwa rahisi, kusamehe inakuwa rahisi kwasababu vyote vyatokana na Mungu.
UKIJUA HAYA UTAKUWA NA FURAHA YA
DAIMA YA WOKOVU
GOD BLESS YOU
Pastor Ibrahim Amasi
ABC - KAHAMA
LivingWord - 2019
" Make a Living "

Mpenzi mfuasi 002

Posted by Savior Ministry at 2:03 AM 0 Comments

Umeshawahi kumsikia BEZALELI mwana wa Uri, mjukuu wa Huri? (Utamsoma zaidi kwenye Kutoka 31, 36 na 39)
Hebu tujifunze kitu kutoka kwake leo.
Huyu ndugu alikuwa ndiye fundi mkuu wa mradi wa hema ya kukutania ambayo Mungu alimwelekeza Musa kuijenga. Alisaidiwa na fundi mwingine anaitwa Oholiabu (huyu tumtunze kwanza pembeni kwa sasa).
Iko hivi, ukisoma sura 24 ya Kutoka, utaona ya kwamba Mungu alimpa Musa, mtumishi wake maelekezo ya kujenga hema. Musa alikuwa anajua details zote za kina za ujenzi wa hema.
Kwa upande mwingine, Bezaleli alikuwa ni mtaalamu, mjuzi, tena mwenye ubora katika ujenzi kama Sayansi na Sanaa.Alikuwa anajua kuliko Musa kwenye hili eneo!
Mfuasi, hasa wewe ambaye umeitwa kwenye nafasi hiyo (achilia mbalia ufuasi wa kishabiki huu). Iko hivi, Mungu amekupa viwekezo ndani yako, ujuzi, utaalamu ambavyo vinapaswa vitumike kwenye kazi na mtumishi uliyewekwa chini yake. Utajikuta kuna maeneo unajua... tena unajua sana... na unamuacha kiongozi wako! Mpenzi, usizuzuke! Ni kawaida kabisa. Wala usione ni ajabu.
Usisahau Musa alikuwa na picha kubwa ya hema nzima ya kukutania mpaka mavazi ya makuhani, mishono, mapazia, materials, vipimo n.k na Bezaleli ana ujuzi wa eneo moja tu ila na kwa kina.
Tumia viwekezo na ujuzi wako wote kwenye ujenzi wa huduma na utumishi huo.
MUHIMU: Unaweza ukatumia ujuzi wako wa kina kuhusiana na eneo husika kutoa MAONI; lakini kamwe usiwe sehemu ya kuyavuruga MAONO ya kazi kubwa kwa ujumla wake.
BE INSTRUCTED!
#wapinduaulimwengu

Mpenzi MFUASI 001

Posted by Savior Ministry at 2:00 AM 0 Comments

Ifike wakati umfuate mtu si kwasababu unapata mshahara, posho, upendeleo, kutajwa, unapewa jukwaa n.k
Ufike wakati umfuate kiongozi kwasababu anakujengea uwezo kuwa JITU... kuua maelfu!
Unakumbuka kwenye pango la Adulamu? Umesoma ile orodha ya sifa ya waliomfuata Daudi pangoni?
1. Hali ya dhiki
2. Madeni
3. Uchungu wa moyo
(1 Sam 22:2)
Kwa Kiswahili ambacho si cha kibiblia - wamechoka, wamechakaa, hawana mbele wala nyuma!
Walimfuata ili awe Jemedari wao!
Kuna kitu watu huwa wanasahau hapa...
Mtu mwingine ambaye alikuwa amechoka na kupigika ni DAUDI MWENYEWE... walimfuata pangoni na si IKULU.
Just imagine, unamfuata kiongozi hana hata nyumba? Hai-make sense... hata ukimuambia mkeo atakuona zuzu kweli.
Daudi mwenyewe maisha yake ni kama mbwa - yuko kwenye mwendo muda wote. Anawindwa na Mfalme Sauli ili auwawe!
Lakini walimfuata. Walimwamini kuwa jemedari. Waliyamimina maisha yao kwake.
Ni hivi:
Kule pangoni Daudi hakuwa anagawa chakula. Wala hakuwa anagawa nyumba na hakuwa anagawa vitu.
Ila kuna namna ukiishi na JEMEDARI (if you rub shoulders with a general) aliyewahi kuua simba, kuua dubu na kuua Goliati anakusababisha ujipate na uwe!
HAYA NDIO MAJINA YA MASHUJAA ALIOKUWA NAO DAUDI... (2 Sam 23:8)
(Ni jumla ya majina ya wanaume 37)
Utagundua, Daudi aliua Goliati mmoja lakini mashujaa wake waliua "magoliati" ya kila rangi!
Just in case:
Naitwa James Kalekwa; mimi ni mfuasi wa Pastor Goodluck Present Kyara.
Asante 🙏🏿

Tuesday, April 25, 2017

HATA NYAKATI ZIWE NGUMU VIPI USIACHE WALA USIOGOPE KUMTOLEA MUNGU (SEHEMU YA II).

Posted by Savior Ministry at 9:28 PM 0 Comments


Mpendwa ninakusalimu katika Jina lipitalo majina yote, Yesu Kristo, Mwana wa Mungu Aliye Hai.

Huu ni mfululizo wa pili katika mfululizo wa masomo ambayo tulianza jana wenye kichwa kinachosema “HATA NYAKATI ZIWE NGUMU VIPI USIACHE WALA USIOGOPE KUMTOLEA MUNGU.”

Katika SEHEMU YA I tuliona jinsi ambavyo fedha huko Misri zilifeli au kwa maneno mengine ilifika mahali ambapo mfumo wa uchumi ambao ulikuwa unategemea fedha (yaani kuuza na kununua) ulishindwa.

Huo mfumo wa uchumi ulipofeli, Wamisri waliutumia mfumo wa kubadilishana mifugo yao ili waweze kupata chakula, lakini nao huo ulifeli.

Baadaye wakaanza kuitoa ardhi yao kwa ajili ya kupata chakula lakini nao ukafeli.

Ndipo Yusufu akaja na mfumo ambao baada ya huo kuingizwa kazini hatuoni ukishindwa tena.

Ulikuwa mfumo wa kupanda na kuvuna.

Walipewa mbegu za kupanda na wakaenda kuzipanda wakapewa sharti kuwa pale watakapovuna watampa Farao asilimia 20 ya walichovuna na hiyo asilimia 80 iliyobaki itakuwa yao kwa ajili ya mbegu na chakula.

Naamini kile walichompa Farao kilikuwa kodi na katika kile walichobaki nacho, mbegu ziliwahakikishia kuwa na kitu katika msimu uliyokuwa unakuja na chakula kiliweza kukutana na mahitaji yao ya wakati ule.

Nilianza hili somo na mfano wa hili jawabu la kiMungu ambalo lilitolewa na Mungu kwa mkono wa Yusufu kwa Wamisri kwa sababu kwenye Agano Jipya la Neema, utoaji unafananishwa na kupanda na kuvuna.

II Wakorintho 9: 6 – 11.

6  Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu. 7 Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu. 8 Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema; 9 kama ilivyoandikwa,
Ametapanya, amewapa maskini,
Haki yake yakaa milele.
10  Na yeye ampaye mbegu mwenye kupanda, na mkate uwe chakula, atawapa mbegu za kupanda na kuzizidisha, naye atayaongeza mazao ya haki yenu; 11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu.

Katika hii mistari ambayo tumenukuu tunaanza kuona akisema apandaye haba atavuna haba naye apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.

Hapa tunaona akifananisha utoaji na upandaji maana hiki kipande cha maandiko kinazungumzia utoaji.

Ili twende sawa lazima kuelewa haya maneno yalityotumika hapa ya ukarimu na uhaba.

Ukarimu na uhaba sio lazima imaanishe uwingi na uchache lakini kwa hakika inamaanisha ulinganifu wa kile ulichotoa kutegemeana na kiwango cha Baraka ambacho Mungu amekubariki.

Nitoe mfano.

Tuna watu wawili A na B na A anayo shilingi elfu kumi na B anayo laki moja.

Katika utoaji A akatoa shilingi elfu tano B akatoa shilingi elfu arobaini.

Ukiangalia uwingi na uchache B atakuwa ametoa zaidi ya A lakini ukiangalia ukarimu na uhaba, A ametoa zaidi ya B maana A ametoa asilimia 50 ya alicho nacho na B ametoa asilimia 40 ya alicho nacho.

Mungu anapoangalia utoaji wetu ndicho anachoangalia.

Je tunatoa sawa na kiwango cha Baraka ambacho ametubariki nacho.

Kwenye maagano yote mawili makuu ya bibilia Mungu aliagiza watu watoe kwa kadiri ya kiwango cha Baraka alichowabariki nacho.

I Wakorintho 16: 1, 2.

1  Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi fanyeni vivyo. 2 Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;

Hapa tunaona Wakorintho wakiagizwa watoe kwa kadiri ya kufanikiwa kwao.

Kwa hiyo haiwezekani sote tukatoa kwa kiasi na kiwango kile kile maana hatujafanikiwa kwa kiwango na kiasi kile kile.

Kumbukumbu la Torati 16: 17.

17 Kila mtu na atoe kama awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya BWANA, Mungu wako, alivyokupa.

Unauona huu mstari?

Kila mmoja wetu anatakiwa atoe kama awezavyo.

Hakuna hata mmoja wetu mwenye udhuru wa kutokutoa.

Kila mmoja wetu atoe awezavyo, kwa kadiri ya Baraka ya Mungu aliyotupa.

Tunapoenda mbele za Mungu kutoa Mungu anajua amembariki na kumfanikisha kila mmoja wetu kwa kiwango gani na hicho ndicho kinachoamua tumetoa kwa ukarimu au uhaba.

II Korintho 8: 12.

12 Maana, kama nia ipo, hukubaliwa kwa kadiri ya alivyo navyo mtu, si kwa kadiri ya asivyo navyo.

Unaona kitu andiko hili linasema mtu wa Mungu?

Kama nia ya kutoa ipo mtu wa Mungu, hukubalika kwa kadiri ya ulivyo navyo na sio kwa kadiri ya usicho nacho.

Kwa hiyo ulicho nacho ndicho kinachoamua kiwango cha utoaji.

Kwa kuwa tumeona kuwa utoaji unafananishwa na upandaji na uvunaji, utakubaliana nami kuwa hakuna mkulima ambaye akishavuna anakula kwanza mavuno yake alafu kile kinachosalia ndicho anakipanda kwa ajili ya msimu ujao wa mavuno.

Yule mkulima kabla hajaanza kula mavuno yake anatenga kwanza atakachopanda na anachagua vizuri mbegu zake.

Kinachotumaliza sana kiuchumi ni kwamba Mungu huwa tunampa masalia baada ya kufanya matumizi yetu yote na tukiwa tunapita kwenye vipindi vigumu ndo mbaya zaidi.

Tunajikuta baada ya kutoa matumizi ya kwetu hakuna kinachobaki cha kumtolea Mungu.

Kumbuka kile Yusufu aliwaambia Wamisri.

Aliwaambia kuwa asilimia 20 wampe Farao alafu hiyo 80 iliyobaki ni yao kwa ajili ya mbegu na chakula.

Katika andiko ambalo tulilinukuu mwanzoni kabisa la I Korintho 9 tunaona maandiko yakituambia kwenye ule mstari wa saba kuwa kila mtu atende kama alivyokusudia moyoni mwake, lakini tukizingatia kile mstari wa 6 kimesema kuhusu uhaba na ukarimu, tusitoe kwa kulazimishwa wala kupangiwa, na wala tusitoe kwa huzuni maana Mungu hupenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.

Ni muhumi sana moyo kukunjuka kabla mkono unaotoa haujakunjuka.

Alafu tunaona andiko likisema kuwa Yeye ampaye mbegu mwenye kupanda na mkate uwe chakula atatupa mbegu za kupanda na kuzizidisha.

Kinachozidishwa ni zile mbegu tunazopanda na katika muktadha ya hili andiko ni zile sadaka tunazotoa kwa kuzingatia kanuni ambazo tumetoka kuziangalia.

Utoaji una nguvu kiasi kwamba kupitia huo Mungu anatujaza kila neema kwa uwingi ili tuwe na riziki za kila namna siku zote na tuweze pia kuzidi sana katika kila tendo jema.

Unaweza kuona unapoacha kutoa kwa sababu kipindi unachopitia ni kigumu, kwanza unafunga majira ya kuvuna maishani mwako maana umefunga majira ya kupanda.

Unaona pia kuwa unazuia kupokea kila neema kwa uwingi kwa hiyo huwezi kuwa na riziki zote siku zote.

Unajikuta kwa sababu ya kuacha kumtolea Mungu inakata mtiririko wa kiMungu wa kukutana na mahitaji yako ya kila siku maana umejitoa kwenye hiyo kanuni kwa kuacha kutoa kwa hiyo kila siku unajikuta unastruggle kama wengine katika nyakati ngumu za kiuchumi.

Mtu wa Mungu hata upitie kipindi kigumu vipi kiuchumi usiache kutoa.

Endelea kuzingatia kanuni ya uhaba na ukarimu tuliyojifunza leo, endelea kutoa kwa kadiri ya kufanikiwa kwako na Baraka za Mungu maishani mwako ili uweze kuendelea kuvuna na kujazwa kila neema kwa uwingi ili usipungukiwe na riziki hata siku moja na uzidi sana katika kila tendo jema.

Mungu akubariki sana.
.

CARLOS RICKY WILSON KIRIMBAI.

WHATSAPP #: +255786312131.

HATA NYAKATI ZIWE NGUMU VIPI USIACHE WALA USIOGOPE KUMTOLEA MUNGU (SEHEMU YA I).

Posted by Savior Ministry at 9:24 PM 0 Comments




Ninakusalimu katika Jina lipitalo majina yote, Yesu Kristo Mwana wa Mungu Aliye Hai.

Bwana Yesu Asfiwe sana.

Leo ninajisikia kwa nguvu sana moyoni mwangu kusema na wewe kuhusu utoaji na japokuwa nitakuwa nikifundisha lakini haya mafundisho sio tu yatakuwa kwa ajili ya kutusaidia kuongezeka ufahamu wa utoaji kwa jinsi ya kiMungu lakini pia huu ufundishaji utakuwa kama ujumbe maalum kwetu kutuhimiza na kututia moyo kwa habari ya umuhimu wa kuendelea kumtolea Mungu hata katika vipindi hivi vigumu (troubled economic times).

Hii sio mara ya kwanza kuwa na vipindi vigumu kiuchumi.

Hata katika bibilia mara kadhaa tunasoma kuwa kulikuwaga na vipindi vigumu sana vya kiuchumi kwa watu na hata kwa familia mbali mbali na pia mataifa.

Tukiangalia maandiko kuna kitu tutakiona:

Mwanzo 47: 15.

15 Fedha zote zilipokwisha katika nchi ya Misri na katika nchi ya Kanaani, Wamisri wote walimjia Yusufu, wakisema, Tupe sisi chakula, kwa nini tufe mbele ya macho yako? Maana fedha zetu zimekwisha.

Kwenye tafsiri ya kiingereza ya New King James Version, hayo maneno “Fedha zote zilipokwisha kwenye nchi ya Misri na nchi ya Kaanani…” yanasomeka “So when the money failed in the land of Egypt and in the land of Canaan,…” ambayo kwa Kiswahili inasomeka “Sasa fedha ziliposhindwa katika nchi ya Misri na nchi ya Kanaani….”

Kwenye tafsiri hiyo ya kiingereza ninapata dhana ya kushindwa kwa mfumo wa kifedha wa Misri na Kanaani.

Hata katika nyakati tunazoishi ninaona kila mahali mfumo wa uchumi wa kifedha ukishindwa.

Mimi sio mtaalamu wa kiuchumi lakini huhitaji kuwa mtaalamu wa kiuchumi kuelewa unapofungulia luninga yako, kusikiliza radio yako, kusoma magazeti na vyombo vya habari kugundua kuwa mifumo ya kifedha kila mahali inashindwa.

Bahati nzuri sio mara ya kwanza kwa mifumo ya fedha kushindwa duniani, na kila ilipotokea Mungu alikuwa na mpango mahususi kwa ajili ya watu Wake kuwakwamua kwenye kushindwa huko kwa mfumo wa kifedha.

Nchi yetu imekumbwa na mdololo wa kiuchumi na mfumuko wa bei ambao umeifanya fedha kuwa ngumu kuipata na kuifanya iongezeke thamani japo katika duru za kimataifa fedha yetu inaonekana kupungua thamani, lakini machoni petu fedha imnekuwa ya thamani sana kwa sababu ya vile ilivyokuwa ngumu kuipata.

Katika nyakati ambazo andiko tulilosoma linatuelezea huko Misri, Mungu alishaona kuwa kutatokea hiyo shida ya kushindwa kwa fedha katika nchi ya Misri na Kanaani na akawa ameandaa suluhisho mapema kwa kumtuma mtu Wake Yusufu katika nchi ile.

Akiwa katika nchi ile Farao aliota ndoto iliyomsumbua ambayo tafsiri yake iliashiria miaka saba ya utele ambayo ilikuwa inakuja kwa nchi ya Misri ikifuatiwa na miaka saba ya njaa na ukame mkali ambayo itafanya ile miaka saba ya utele isahaulike.

Wakati ilipokuwa inasemekana kuwa fedha zimeshindwa katika nchi ya Misri nan chi ya Kanaani, ilikuwa kipindi ambacho njaa na ukame vimeshaanza kuuma.

Ninapoendelea kusoma hiyo habari nimeshtushwa kidogo na suluhisho ambalo lilitolewa na Yusufu kwa ajili ya ile hali ambayo ilikuwa inaendelea.

Watu wa Misri walipomfuata baada ya fedha kushindwa na kukosa uwezo wa kununua tena chakula (loss of purchasing power), Yusufu akawaambia Wamisri wawatoe wanyama wao badala ya chakula.

Kwa hiyo badala ya kutoa fedha ambazo zimeshindwa, wakaanza kutoa mifugo yao.

Lakini hata hao wanyama wakaisha maana hata uwe na akiba kubwa kiasi gani, kama huzalishi unatumia tu, hiyo akiba nayo itaisha.

Kwa hiyo akiba yao ya wanyama nayo ikaisha.

Ikafika mahali ili Wamisri wapate chakula ilibidi waachie ardhi yao kwa Farao ili badala ya ardhi wapate chakula.

Hakika hizi zilikuwa nyakati ngumu sana kiuchumi.

Lakini pia hata hiyo ardhi yote waliyokuwa nayo ikaisha.

Nilitaka uone kuwa mfumo wa fedha ulishindwa, mfumo wa biashara ya mabadilishano (barter trade) nao ulishindwa na pia hata kutoa ardhi kwa ajili ya kupata chakula nao ukashindwa.

Baada ya hii mifumo mitatu yote kushindwa, ndipo sasa Yusufu akaja na wazo ambalo lingekuwa suluhisho mpaka pale ile hali ya njaa na ukame itakapopita.

Aliwapa mbegu za kwenda kupanda.

Nilijiuliza sana, hivi hizi mbegu wanaenda kuzipandaje wakati ni kipindi cha njaa na ukame?

Ilinisumbua sana.

Nikajua kuwa hili lilikuwa suluhisho la kiMungu kwa ajili ya tatizo lilokuwepo.

Akawaagiza wapande zile mbegu na wakati wa mavuno asilimia 20 wampe Farao na hizo 80 zilizobaki ziwe zao kwa ajili ya mbegu na chakula.

Baada ya hapo hatuoni tena waMisri wakimrudia tena Yusufu.

Fedha zilishindwa, wanyama wao walishindwa, ardhi yao ilishindwa ila mfumo wa kupanda na kuvuna ukawa ndo suluhisho la mdololo wa uchumi ambao uliipata Misri.

Husomi tena katika maandiko Wamisri wakija kulalamika kuwa hawana chakula.

Hii hekima ya kupanda na kuvuna ikawa ndo suluhisho la kudumu.

Panda katika nchi, vuna, mpe Farao asilimia 20 na wao wenyewe watumie ile 80 iliyobaki kwa mbegu na chakula.

Katika sehemu inayofuata tutaendelea kufuatilia hii hekima ya Mungu ambayo ni dawa ya vipindi vigumu vya kiuchumi.

Lakini inatosha kusema kuwa kutomtolea Mungu katika vipindi vigumu vya kiuchumi ni kuweka tumaini lako katika fedha zisizo yakini na zitakuja kushindwa tu.

Ila tukijua ni kwa jinsi gani tunapaswa kumtolea Mungu katika vipindi hivi vigumu tutavuka kama Wamisri wao walivyovuka katika kipindi kigumu cha mdololo wa kiuchumi.

Nimalizie kwa kukupa haya maandiko:

Mithali 11: 24, 25.

24 Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi;
Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji.
25  Nafsi ya mtu mkarimu itawandishwa;
Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe.

Luka 6: 38.

38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.

Mungu akubariki sana.

CARLOS RICKY WILSON KIRIMBAI.

WHTASAPP #: +255786312131.

Thursday, April 20, 2017

UJUE MSAADA WA ROHO MTAKATIFU KATIKA MAOMBI.

Posted by Savior Ministry at 10:24 PM 4 Comments

UTANGULIZI:

Hili somo limelenga kuwasaidia wale ambao wanashindana (struggle) katika maisha yao ya maombi maana ni kama ndani yao wanatamani kuwa na maisha imara, thabiti na yenye ufanisi ya maombi lakini vipo vitu vinawazuia.

Mungu hategemei wewe uyajenge maisha yako ya maombi kwa nguvu na uweza wako mwenyewe na ndiyo maana anasema katika neno Lake:

Zekaria 4: 6.

6Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la BWANA kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema BWANA wa majeshi.

Na pia ndo maana neno Lake linasema tena sehemu nyingine:

Zaburi 104: 30.

Waipeleka roho yako, wanaumbwa,
Nawe waufanya upya uso wa nchi. 

Mungu anampeleka Roho Wake maishani mwetu kwa kusudi la kuyaumba upya maisha yetu ya maombi na kufanya upya maisha yetu ya maombi.


Baada ya kusema maneno hayo ya utangulizi, ili uweze kusaidiwa katika maisha yako ya maombi lazima kwanza ukubali kuwa unao udhaifu katika eneo hilo kama maandiko yasemavyo:

Warumi 8: 26.

18Ebr26Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

Tunaona wazi kuwa Roho Mtakatifu anatusaidia katika udhaifu wetu wa kutoweza kuomba itupasavyo kuomba.

Tena maandiko yanasema tena sehemu nyingine:

Ayubu 26: 2.

2 Jinsi ulivyomsaidia huyo asiye na uwezo!
Jinsi ulivyouokoa mkono usio na nguvu!

Kwa hiyo kama huna uwezo wa kuyanidhamisha maisha yako ili kujenga maisha imara na yenye ufanisi na tija ya maombi Mungu atakusaidia kufanya hivyo kwa Roho Wake Mtakatifu.

Tunasoma tena katika maandiko:

Waefeso 6: 18.


18kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;

Tunaambiwa wazi na bayana kuwa kila tusalipo na tuombapo tufanye hivyo katika Roho au kwa maneno mengine kwa msaada wa Roho Mtakatifu.

Mtume Yuda naye anatuambia:

Yuda 1: 20.

20Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu,

Tunaona tena mkazo ukiwekwa wa kuomba katika Roho Mtakatifu au kwa maneno mengine kwa msaada wa Roho Mtakatifu.

Yesu alipo wakuta wanafunzi Wake wamelala baada ya kushindwa kusimama naye katika maombi saa ambayo alihitaji sana wasiamame Naye aliwaambia:

Mathayo 26: 41.

41Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.

Changamoto kubwa ambayo mwamini atakutana nayo katika kuyajenga maisha thabiti, imara na yenye ufanisi ya maombi ni udhaifu wa mwili. 

Ndani katika roho yake anataka kuomba lakini mwili wake unamzuia kuomba. 

Hapo ndipo msaada wa Roho Mtakatifu unapohitajika sana.

Maandiko yanatumabia:

Zaburi 80: 18.

18Basi hatutakuacha kwa kurudi nyuma;
Utuhuishe nasi tutaliitia jina lako.

Daudi alijua wazi ili aweze kuliitia Jina la Bwana lazima kwanza ahuishwe.

Kuhuishwa huko ambako kutatupelekea tuweze kuliitia Jina la Bwana huwezekana kwa kazi ya Roho Mtakatifu maishani mwetu.

Mungu kwa Roho Wake Ndiye atuhuishaye ili tuweze kuliitia Jina Lake.

Warumi 8: 11.

11Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu.

Pindi ujuapo unatakiwa kuomba lakini unasikia udhaifu katika mwili muombe Mungu akuhuishe kwa Roho Wake ili uweze kuomba.

Lakini pia Mungu kwa Roho wake hutusaidia lugha ya kuombea pia.

Sefania 3: 9.

9Maana hapo ndipo nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi, wapate kuliitia jina la BWANA, wamtumikie kwa nia moja.

Ninaamini kuwa lugha hiyo safi ambayo kwayo twaliitia Jina la Bwana ni lugha ya maombi ya Roho Mtakatifu ambayo ni kunena kwa lugha mpya katika maombi au kunena katika maombi kama Roho anavyotujalia kutamka.

Hapa ndipo palipo na umuhimu mkubwa sana wa kujazwa na Roho Mtakatifu ili uweze kuomba kwa lugha hii.

Unapoomba kwa kutumia lugha hii safi unakuwa na mazungumzo ya moja kwa moja na Mungu kupitia roho yako kwa lugha safi hiyo ya Roho Mtakatifu.

I Korintho 14: 2.

2Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho yake.

Lugha hii safi ya maombi sio tu inakuwezesha kuongea moja kwa moja na Mungu bali pia inakuwezesha kuyaomba mambo ya siri na ya mafumbo kwa upeo ambao ufahamu wako wa kawaida usingeweza kuomba.

Unapoomba kwa lugha hii safi ya Roho Mtakatifu, roho yako kwa msaada wa Roho Mtakatifu inaomba na akili zako hazielewi hasa kinachoendelea ila unakuwa unaomba kwa ufanisi mkubwa sana.

I Korintho 14: 14, 15.

14Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda. 15Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia.

Mwisho kabisa niseme kuwa Roho Mtakatifu hutusaidia kuomba kwa kutupa ajenda au dondoo za kuombea maana Yeye ndo anajua kile ambacho Mungu yupo tayari kufanya kwa ajili yetu wakati huo kwa hiyo atatuwekea moyoni kile cha kuombea ili tuombapo tuombe sawa na mapenzi ya Mungu kwa ajili yetu wakati huo.

I Korintho 2: 12.

12Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.

Anaposema tupate kujua tuliyokirimiwa na Mungu ninaamini inatusaidia kujua saa hiyo na katika majira hayo Mungu yupo tayari kufanya nini kwa ajili yetu ili tukiombe hicho.

Maandiko yanasema:

Zekaria 10: 1.

1 Mwombeni BWANA mvua wakati wa masika, naam, BWANA afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni.

Kwanini uanze kumwomba Mungu mvua toka kipindi cha kiangazi wakati Mungu hatajibu hayo maombi mpaka kipindi cha masika?

Si usubiri masika ndo umwombe Mungu mvua Naye atajibu hayo maombi maana yameombwa kiusahihi katika msimu sahihi?

Vivyo hivyo katika maisha yetu kuna wakati sahihi na majira sahihi ya Mungu kufanya mambo tofauti tofauti.

Roho Mtakatifu anatusaidia kuomba kwa kuzingatia majira na misimu ambayo Mungu yupo tayari kufanya mambo mbali mbali maishani mwetu.

MUNGU AKUBARIKI SANA.

Mchungaji na Mwalimu Carlos R W. Kirimbai

KUKAZA KUMPENDA MUNGU

Posted by Savior Ministry at 10:08 PM 0 Comments



Zaburi 91:14-16
“Kwakua amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, kwa kuwa amenijua jina langu…”

Unaposema KUKAZA ni kinyume cha neno KULEGEA
Unapo KAZA kumpenda MUNGU maana yake unaongeza bidii kwaajili ya MUNGU, unaweka bidi kujifunza
Yeremia 48:10 Kufanya kazi kwa ULEGEVU ni Chanzo cha LAANA Ukilegea KUKAZA KUMPENDA BWANA unajitafutia LAANA.
NAMNA YA KUKAZA KUMPENDA MUNGU
KUKAZA tunamaanisha kuwa na JUHUDI za makusudi, kuwa na mipango na mikakati kabambe ili kumkaribia MUNGU aliye hai.
(wengi wameokoka lakini hawana juhudi za kumkaribia MUNGU baada ya kuwa umeokoka ni wakati wa wewe kuwa KARIBU na Mungu anasema nikaribieni mimi name nitawakaribia)
  •   KUSOMA NENO LA MUNGU
Unapokua unakaza KUMPENDA BWANA, kumbuka yeyote anaye nikaribia sitomtupa kamwe.
Umesumbuka mda mrefu, umeangaika mda mrefu lakini AMUA leo KUKAZA KUMPENDA MUNGU ili yeye aingilie kati katika maisha yako.
Panga Ratiba yako katika Kusoma NENO LA MUNGU, weka mipango ya KUONGEZA MAARIFA YA BWANA.
Lazima ukaze kutafuta NENO LA BWANA, biblia inasema siku zina kuja ambapo watu watatafuta NENO LA MUNGU na hawataliona

  • KUOMBA KWA BIDII
Lazima ujifunze kukaza kumpenda MUNGU katika SALA. 1 Petro 4:7 “mwisho wa Mambo  umekaribia basi iweni na aKili mkeshe katika sala”. Huu si wakati wa kuomba dakika Moja, ni wakati wa kukesha katika SALA.
Wakati mwingie si rahisi kuomba peke yako pata lifti kwa waombaji, jiunge kwenye vikundi vya maombi, nenda kwenye Mikesha, jinyime kula funga, hivi vitakusaidia kuwa karibu na MUNGU.
Acha kuomba kwasababu unataka kula, au kulala, au ili uponywe, unamwomba MUNGU ili aweze kuwa pamoja nawe njiani. KAZA KUMPENDA BWANA kuwa na bidii katika MAOMBI.

  •   USHUHUDA WAKO

Kaza kuwa na bidii katika ushuhuda wako, Daudi anasema wanao kutumaini wasiaibishwe kwaajili yangu eebwana wa majeshi. Wapo watu ambao hawapo makini na ushuhuda wa kwao, mtu anasema mtumishi wa Mungu, mimi ni muhubiri lakini matendo yake ni kinyume na kile anachokisema mtu huyu hawezi kukaza kumpenda MUNGU. Unapokaza kumpenda MUNGU ni lazima ushuhuda watu wanapo kutazama na kukuona wamuone MUNGU anaishi ndani yako, waone NGUVU ya Mungu inaishi ndani yako, waone Roho wa Bwana yuko ndani yako bila mashaka kabisa yaani watamani kuokolewa kwasababu ya maisha unayo yaishi. Wewe si wa ulimwengu huu wewe ni waulimwengu ujao unapokua kwenye nchi ya kwako unapaswa kuishi maisha ya nidhamu. Kaza katika kuwa na ushuhuda mzuri. Kuna mahali haupaswi kwenda au kushika maana vita haribu ushuhuda wako.
4.       KATIKA UAMINIFU WOTE (MTUMIKIE MUNGU KWA MALI ZAKO)
Mtumikie Bwana kwa mali yako, mali zako. Kwa habari ya fungu la kumi kaza kumpenda Bwana, acha visingizio kwa habari ya fungu la Kumi. Mtu mmoja alitoa mfano wa kutoa fungu la kumi eti alikua amebeba alafu kibaka akamuibia je atakua amesamehewa lile fungu la kumi? Labda tufikiri kwa style ingine je ulikua umebeba ada ya shule ya mwanao alafu ikaibiwa je utakua umesamehewa ada? Tumia nguvu zako kumtumikia Bwana. (Siku za Mwisho upendo wa wengi utapoa…) kumbuka tupo katika mashindano yeye ni Mungu wa wengi ukiringa ana watu wengi.


  •   KUTENDA KAZI YA MUNGU

Agizo kuu la Yesu ni kuihubiri injili, bilbia inasema enendeni ulimwengu wote kuihubiri Injili ya Bwana. Jirani zako, rafiki zako wote wanatamani kusikia habari za Yesu lakini wewe hauwaambii huko siyo kukaza Kumpenda MUNGU. Ukikaza kumpenda Mungu hata lugha yako inabadilika mara zote unafikiria habari ya Bwana.

MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA KUKAZA KUMPENDA MUNGU.
1.       Kaza katika Kujifunza na kusoma Neno lake.
2.       Kaza katika kuomba na kutafuta uso wa Bwana.
3.       Kaza katika kujenga ushuhuda mzuri mbele za Mungu na wanadamu
4.       Kaza katika uaminifu wote
5.       Kaza katika kutenda kazi ya Mungu kwa uaminifu.
FAIDA ZA KUKAZA KUMPENDA MUNGU
·         Mungu atakuokoka

The Savior Ministry Live Chat

© 2016 Savior Ministry.
Powered by Themes24x7 .
back to top