Zaburi 91:14-16
“Kwakua amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu,
kwa kuwa amenijua jina langu…”
Unaposema KUKAZA ni kinyume cha neno KULEGEA
Unapo KAZA kumpenda MUNGU maana yake unaongeza bidii
kwaajili ya MUNGU, unaweka bidi kujifunza
Yeremia 48:10 Kufanya kazi kwa ULEGEVU ni Chanzo cha LAANA
Ukilegea KUKAZA KUMPENDA BWANA unajitafutia LAANA.
NAMNA YA KUKAZA KUMPENDA MUNGU
KUKAZA tunamaanisha kuwa na JUHUDI za makusudi, kuwa na
mipango na mikakati kabambe ili kumkaribia MUNGU aliye hai.
(wengi wameokoka lakini hawana juhudi za kumkaribia MUNGU
baada ya kuwa umeokoka ni wakati wa wewe kuwa KARIBU na Mungu anasema
nikaribieni mimi name nitawakaribia)
- KUSOMA NENO LA MUNGU
Unapokua unakaza KUMPENDA BWANA, kumbuka yeyote anaye
nikaribia sitomtupa kamwe.
Umesumbuka mda mrefu, umeangaika mda mrefu lakini AMUA leo
KUKAZA KUMPENDA MUNGU ili yeye aingilie kati katika maisha yako.
Panga Ratiba yako katika Kusoma NENO LA MUNGU, weka mipango
ya KUONGEZA MAARIFA YA BWANA.
Lazima ukaze kutafuta NENO LA BWANA, biblia inasema siku
zina kuja ambapo watu watatafuta NENO LA MUNGU na hawataliona
- KUOMBA KWA BIDII
Lazima ujifunze kukaza kumpenda MUNGU katika SALA. 1 Petro
4:7 “mwisho wa Mambo umekaribia basi
iweni na aKili mkeshe katika sala”. Huu si wakati wa kuomba dakika Moja, ni
wakati wa kukesha katika SALA.
Wakati mwingie si rahisi kuomba peke yako pata lifti kwa
waombaji, jiunge kwenye vikundi vya maombi, nenda kwenye Mikesha, jinyime kula
funga, hivi vitakusaidia kuwa karibu na MUNGU.
Acha kuomba kwasababu unataka kula, au kulala, au ili
uponywe, unamwomba MUNGU ili aweze kuwa pamoja nawe njiani. KAZA KUMPENDA BWANA
kuwa na bidii katika MAOMBI.
- USHUHUDA WAKO
Kaza kuwa na bidii katika ushuhuda wako, Daudi anasema wanao
kutumaini wasiaibishwe kwaajili yangu eebwana wa majeshi. Wapo watu ambao
hawapo makini na ushuhuda wa kwao, mtu anasema mtumishi wa Mungu, mimi ni
muhubiri lakini matendo yake ni kinyume na kile anachokisema mtu huyu hawezi
kukaza kumpenda MUNGU. Unapokaza kumpenda MUNGU ni lazima ushuhuda watu wanapo
kutazama na kukuona wamuone MUNGU anaishi ndani yako, waone NGUVU ya Mungu
inaishi ndani yako, waone Roho wa Bwana yuko ndani yako bila mashaka kabisa
yaani watamani kuokolewa kwasababu ya maisha unayo yaishi. Wewe si wa ulimwengu
huu wewe ni waulimwengu ujao unapokua kwenye nchi ya kwako unapaswa kuishi
maisha ya nidhamu. Kaza katika kuwa na ushuhuda mzuri. Kuna mahali haupaswi
kwenda au kushika maana vita haribu ushuhuda wako.
4.
KATIKA UAMINIFU WOTE (MTUMIKIE MUNGU KWA MALI
ZAKO)
Mtumikie Bwana kwa mali yako, mali zako. Kwa habari ya fungu
la kumi kaza kumpenda Bwana, acha visingizio kwa habari ya fungu la Kumi. Mtu
mmoja alitoa mfano wa kutoa fungu la kumi eti alikua amebeba alafu kibaka
akamuibia je atakua amesamehewa lile fungu la kumi? Labda tufikiri kwa style
ingine je ulikua umebeba ada ya shule ya mwanao alafu ikaibiwa je utakua
umesamehewa ada? Tumia nguvu zako kumtumikia Bwana. (Siku za Mwisho upendo wa
wengi utapoa…) kumbuka tupo katika mashindano yeye ni Mungu wa wengi ukiringa
ana watu wengi.
- KUTENDA KAZI YA MUNGU
Agizo kuu la Yesu ni kuihubiri injili, bilbia inasema
enendeni ulimwengu wote kuihubiri Injili ya Bwana. Jirani zako, rafiki zako
wote wanatamani kusikia habari za Yesu lakini wewe hauwaambii huko siyo kukaza
Kumpenda MUNGU. Ukikaza kumpenda Mungu hata lugha yako inabadilika mara zote
unafikiria habari ya Bwana.
MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA KUKAZA KUMPENDA MUNGU.
1.
Kaza katika Kujifunza na kusoma Neno lake.
2.
Kaza katika kuomba na kutafuta uso wa Bwana.
3.
Kaza katika kujenga ushuhuda mzuri mbele za
Mungu na wanadamu
4.
Kaza katika uaminifu wote
5.
Kaza katika kutenda kazi ya Mungu kwa uaminifu.
FAIDA ZA KUKAZA KUMPENDA MUNGU
·
Mungu atakuokoka
0 Comments: