Friday, January 3, 2020

Mpenzi mfuasi 002

Posted by Savior Ministry at 2:03 AM 0 Comments

Umeshawahi kumsikia BEZALELI mwana wa Uri, mjukuu wa Huri? (Utamsoma zaidi kwenye Kutoka 31, 36 na 39)
Hebu tujifunze kitu kutoka kwake leo.
Huyu ndugu alikuwa ndiye fundi mkuu wa mradi wa hema ya kukutania ambayo Mungu alimwelekeza Musa kuijenga. Alisaidiwa na fundi mwingine anaitwa Oholiabu (huyu tumtunze kwanza pembeni kwa sasa).
Iko hivi, ukisoma sura 24 ya Kutoka, utaona ya kwamba Mungu alimpa Musa, mtumishi wake maelekezo ya kujenga hema. Musa alikuwa anajua details zote za kina za ujenzi wa hema.
Kwa upande mwingine, Bezaleli alikuwa ni mtaalamu, mjuzi, tena mwenye ubora katika ujenzi kama Sayansi na Sanaa.Alikuwa anajua kuliko Musa kwenye hili eneo!
Mfuasi, hasa wewe ambaye umeitwa kwenye nafasi hiyo (achilia mbalia ufuasi wa kishabiki huu). Iko hivi, Mungu amekupa viwekezo ndani yako, ujuzi, utaalamu ambavyo vinapaswa vitumike kwenye kazi na mtumishi uliyewekwa chini yake. Utajikuta kuna maeneo unajua... tena unajua sana... na unamuacha kiongozi wako! Mpenzi, usizuzuke! Ni kawaida kabisa. Wala usione ni ajabu.
Usisahau Musa alikuwa na picha kubwa ya hema nzima ya kukutania mpaka mavazi ya makuhani, mishono, mapazia, materials, vipimo n.k na Bezaleli ana ujuzi wa eneo moja tu ila na kwa kina.
Tumia viwekezo na ujuzi wako wote kwenye ujenzi wa huduma na utumishi huo.
MUHIMU: Unaweza ukatumia ujuzi wako wa kina kuhusiana na eneo husika kutoa MAONI; lakini kamwe usiwe sehemu ya kuyavuruga MAONO ya kazi kubwa kwa ujumla wake.
BE INSTRUCTED!
#wapinduaulimwengu

Share This Post

Get Updates

Subscribe to our Mailing List. We'll never share your Email address.

0 Comments:

The Savior Ministry Live Chat

© 2016 Savior Ministry.
Powered by Themes24x7 .
back to top