Tuesday, January 3, 2017

JARIBU KUFANYA NA YESU MWAKA HUU 2017

Posted by Savior Ministry at 7:50 AM 0 Comments


Bwana Yesu asifiwe!

Mara nyingi katika maisha yetu huwa tunafeli na kukosea shuleni,kazini,kwenye biashara,katika ndoa.n.k Hii ni kwa sababu tunategemea akili zetu na maarifa yetu wenyewe.
Ebu tusome maandiko

 Yohana 15:5
5 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.

Hapa tunapata majibu kwanini hatufanikiwi sababu Neno la Mungu ni amini na kweli nalo lasema kwamba pasipo yeye(Yesu) sisi hatuwezi kufanya neno lolote...hii ina maana wakati wowote tunapomuweka nje ya mipango na maamuzi yetu...tumeamua kufeli au kushidwa.

Yamkini ulitenda na kufanya mengi mwaka jana na hayakufanikiwa sababu ulimuacha Yesu nje ila mwaka huu mualike ufanye naye na utaona mafanikio tele.

Utaona ukisoma Yohana 21:1-11
Utaona wanafunzi walivua samaki wakiwa peke yao na kukosa samaki lakini alivyokuja Yesu walipata samaki...
Kwanini?
Kwa sababu Yesu alivyokuja aliwapa Direction(MWELEKEO) aliwaambia katika mstari wa 6 tupeni jarife katika upande wa kuume....
Sijui unaona kitu hapo!!!

Yeye Yesu akiwa na wewe atakupa mwelekeo wapi upite wapi usipite nani uhusiane nae nani usihudiane nae...
Tunamuhitaji huyu Yesu maana bila mwelekeo hatutaweza fikia tunapotaka kufika.
Biblia inasema pasipo maono watu huacha kujizuia.
Yesu anaijua kesho Yetu ebu mkabidhi njia zako aziongoze...mwambie atwae miguu yako kwa uongozi wake...pasipo yeye mwenye maono tutashidwa kujizuia na kufanya yasiyo tupasa na hivyo kushidwa kufikia hatma zetu...

Mkabidhi Bwana njia zako pia umtumaini naye atafanya.

Mungu akubariki.

Share This Post

Get Updates

Subscribe to our Mailing List. We'll never share your Email address.

0 Comments:

The Savior Ministry Live Chat

© 2016 Savior Ministry.
Powered by Themes24x7 .
back to top