Bwana Yesu asifiwe, ninamshukuru Mungu kwa muda huu, na
nafasi hii adimu ya kuzungumza na wewe kwa njia ya maandishi juu ya NIA
YA DHATI YA YESU DUNIANI, hii inakuhusu wewe uliyeokoka, ambaye
hujaokoka na ambaye uliokoka lakini ukarudi nyuma.
Ukweli ni kwamba Mungu anafanya kazi na wote wampendao, nao
ndio watendao sheria zake na kuzifuata, hao ndio waongozwao na Roho
wake, uwepo wake unakuwa juu yao.
Lakini dhambi baada ya kuingia duniani ilituondolea nafasi
tuliyokuwa tumepewa baada ya Adamu kula tunda alilokatazwa, hivyo
ikambidi Yesu aturejeshee ile nafasi kupitia Damu yake inenayo mema.
Leongo la ujumbww huu ni kukutazamisha hii mistari michache
ili uone nia ya dhati ya Yesu ya kuturejeshea nafasi, embu sema NAFASI,
NAFASI.
Neno la Mungu katika biblia linatupa uhakika ya kuwa tunapokuwa katika Kristo Yesu tunapewa nafasi ya kuwa
1. WAFALME
2. MAKUHANI
2. MAKUHANI
Hizi kimsingi ni nafasi mbili tofauti zinazofanya kazi tofauti tofauti.
Ufunuo 5:9-10
''Ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na jamaa na taifa, ukawfanya kuwa UFALME na MAKUHANI kwa Mungu wetu, nao wanamiliki juu ya nchi''
''Ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na jamaa na taifa, ukawfanya kuwa UFALME na MAKUHANI kwa Mungu wetu, nao wanamiliki juu ya nchi''
Kwa maandiko haya yananipa picha kubwa ya uhalisia ya kuwa mambo kadhaa
Jambo la kwanza.
Nafasi ilipatikana kwa njia Damu ya Yesu iliyotumika kama
njia ya Transaction ili upate NAFASI, biashara ilotumika upate hiyo
nafasi ni DAMU ya Yesu.
Jambo la pili.
Kila anayeitwa Mtu kutoka kabila lolote YESU hakwepeki,
Kwa nini hakwepeki? Ile Damu haikubagua Kabila, Dini, Dhehebu, wala Rangi, wote tulinunuliwa kwa hiyo Damu,
Ukimkubali tu unapewa nafasi ya UFALME na ukuhani kwa ajili ya kumiliki na kitawala kwa njia ya Yesu Kristo.
Ufunuo 1:5-6
''..... Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake, na kutufanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu.
''..... Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake, na kutufanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu.
kimsingi katika hali ya kawaida kufanyika mfalme na kuhani
kwa wakati mmoja ni jambo kubwa na la heshima sana ambayo Mungu anampa
mtu katika ya watu wengine ambao hawajaokoka ili huyo mtu atawale na
kumiliki na Kristo.
Sisi ni warithi pamoja na kristo Yesu.
Sisi ni watawala pamoja na Kristo Yesu.
Hatukustahili ili tulistahilishwa kwa agano la Damu ya Yesu ili tumiliki na kutawala na Kristo Yesu,
Baada ya dhambi kuingia ulimwenguni ile nafasi tuliyokuwa
tumepewa kupitia Adam wa kwanza aliipoteza ndiyo maana akafukuzwa kwenye
bustani ya EDEN, hii ikaondoa uhalali wa kumiliki na kutawala.
Usitegemee umetenda dhambi Halafu utukufu wa Bwana uwe juu yako, IKABODI.
Adam wa pili amerejesha sasa nafasi iliyokuwa imepotea.
Kama hujaokoka wokovu upo kwa ajili yako, mpokee Yesu awe
Bwana na mwokozi wa maisha yako, usikubali kuingia mwaka 2016 ukiwa bado
hujaokoka, wokovu ni sasa na si kesho, OKOKA LEO.
Na Mwl David Sedekia
P. O. Box 1652
Dodoma
Tanzania.
P. O. Box 1652
Dodoma
Tanzania.
0 Comments: