Kwa Neema ya MUNGU ametupatia tena, mwaka huu 2016 ni mwaka ambao Theme ya Mwaka Mzima as Savior Ministry tutakua nayo ni "UTOSHELEVU WETU WATOKA KWA MUNGU" Ukipitia 2 Wakorith 3:5 utaona. laini pia mwaka huu kila jambo ambalo MUNGU ameliahidi katika NENO lake litakua kwaajili yako pia kinacho hitajika toka kwako ni kuwa CONNECTED.
Mwaka huu Mpya unapokuja mbele yako uwe na wakika kwanza MUNGU amekuamini, sasa ni sehemu yako kufanya katika viwango vya kimbingu. Mungu amekuamini tena kwaajili ya wewe kumzalia MATUNDA. Yohana 15:1-10
YESU ni MZABIBU
WEWE ni TAWI
MUNGU ni MKULIMA
TAWI linahitaji UHUSIANO Mzuri sana na MZABIBU ili lipate KUZAA. Unajua Tawi lisipoza MKULIMA haitaji kukata MTI MZIMA anaondoa TAWI.
Mstari wa 5 anasema "Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huza sana; maana pasipo mimi ninyi HAMWEZI KUFANYA NENO LOLOTE"
Alafu ukiruka mpaka mstari wa 7 anasema "Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yen, omeni mtakalo lolote nanyi mtatendewa"
sasa unaweza ukaona namna TAWI linahitaji MZABIBU ili kufanya VIZURI. Unacho cha kufanya Mwaka huu 2016.
Happy NEW YEAR 2016...
Waweza wasiliana nasi au kutujoin kwa kuclick SHIRIKIANA NASI
Be Blessed!!!
2016 "Utoshelevu wetu watoka kwa MUNGU"
0 Comments: