Saturday, May 4, 2013

Tuitafsiri 666

Posted by Savior Ministry at 10:13 PM 0 Comments
666

Leo nilikuwa nasoma mtandaoni juu ya kupitishwa kwa mswada wa Afya wa Rais Obama wa USA kuwa sheria ikanilazimu kusoma tena Ufunuo 13: 15 – 18 ili kuona kama unabii wa huo wa Yohana ndiyo huu wa sasa USA?. Hebu soma kwanza habari yenyewe nimejaribu kuitafsiri hapa kama ifuatavyo;

“Namba 666 = ni alama ya MPINGA KRISTO (Soma Ufunuo wa Yohana). Bunge la Marekani limepitisha Mpango wa Afya wa rais Obama kuwa sheria. Utekelezaji wake utaanza tarehe 23/03/ 2013. Sheria hii itahitaji Wamarekani wote kupandikizwa Kifaa cha mawimbi ya redio (Radio Frequency Identification (RFID) chip) ili kunufaika na mpango huu wa afya na kupata dawa. Kifaa hicho kitawekwa kwenye paji la uso au kwenye mkono na kitaunganishwa na akaunti za benki za raia mhusika.”

Jambo hili kwa [maoni yangu] linatimiza unabii uliomo katika kitabu cha Ufunuo 13:15-18 kuhusiana na ALAMA YA MNYAMA! Mwenzangu bado unatilia mashaka juu ya NYAKATI ZA MWISHO? KAA TAYARI! Wakati wa mavuno u karibu sana! Ufunuo 13 nadhani umeanza kuonekana wazi mbele yetu [Marekani si mbali]. Ingawa nadhani wengi hatujapata habari hizi na hata zitakapokuja rasmi pengine hatutajishughulisha kujiuliza maswali haya;

1. Kwa nini hiki kifaa kiwekwe kwenye maeneo yaleyale ya mwili ambayo Biblia imeonyesha kupitia Ufunuo. Kwa nini kifaa kiwekwe kwenye paji la uso au mkononi na siyo mahali pengine?

2. Kwa nini kifaa hicho cha mawimbi kiunganishwe na akaunti yako ya benki? Kumbuka Biblia inasema hautanunua wala kuuza bila kuwa na alama hiyo ya mnyama [asomaye na afahamu]. Na hebu fikiria kwa nini hicho kifaa kiwe na taarifa zako za fedha. Kinachoniumiza moyo ni kuwa watu wengi ndani ya makanisa wanadhani zile nyakati zingali bado sana na Yesu akija sasa wengi wetu tutaangamia? Najua wengi hapa tutasema ni maendeleo ya kiteknolojia lakini si vibaya tukihusisha na maandiko kisha tukajitathmini Je! Sisi tuko wapi leo.

–Moses


Share This Post

Get Updates

Subscribe to our Mailing List. We'll never share your Email address.

0 Comments:

The Savior Ministry Live Chat

© 2016 Savior Ministry.
Powered by Themes24x7 .
back to top